Balozi Fulgence kazaura ateuliwa tena kuwa mkuu wa chuo kikuu cha Dar es salaam


Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Balozi Fulgence Kazaura akimtunuku PhD Waziri wa ujenzi Dk. John Magufuli katika mahafali iliyopita ya Chuo Kikuu hicho


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Balozi Fulgence Kazaura kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kipindi kingine cha miaka minne.


Taarifa iliyotolewa leo, Jumanne, Oktoba 18, 2011, na Katibu Mkuu Kiongozi Phillemon Luhanjo imesema kuwa uteuzi huo unaanza mara moja leo hii.


Balozi Kazaura alikuwa Mkuu wa Chuo hicho katika kipindi kilichopita kilichoishia Julai, mwaka huu, 2011.


Imetolewa na:


Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.


18 Oktoba, 2011

Post a Comment

ads by blogger

Follow Us

Hot in week

BLOG ZINGINE

BLOG OWNER

BLOG OWNER
MESHACK JACKSON

Side Ads

Instagram

JOIN US ON TWITTER

Text Widget

Millard Ayo – Official Website

item