CHOMBEZO: GUBERI LA KIMANYEMA


MTUNZI: INNOCENT A. NDAYANSE (ZAGALLO)

SIMU: 0713 59 35 46/0755 04 05 20


SEHEMU YA PILI



Sharifa alilainika kama mboga ya bamia. Akakamatwa kiuno na kuvutiwa kwenye kitanda cha mama yake. Wakashiriki dhahama. Naam, hawakujua ni ngoma ipi waliyocheza pale kitandani. Kama ni sindimba, basi ilikuwa sindimba kweli. Kama ni Mduara basi ulikuwa ni Mduara halisi. Kama ni Mugongomugongo, ilitisha. Chumbani kwa Mama Kadala, kitandani kwa Mama Kadala, na mtoto wa Mama Kadala!

Kiwembe! Kabalehe kwenye kifua cha Mama Kadala, na sasa anafanya mazoezi kwenye mwili wa mtoto wa Mama Kadala! Kwenye kitanda kilekile!

Huo ulikuwa ni mwanzo tu, mwanzo uliofungua ukurasa mpya wa uhusiano baina yao. Penzi likawanogea. Awali ilikuwa ni siri, siri iliyofichika, lakini hatimaye minong’ono ikaanza kuzagaa mitaani. Siri hiyo ilianza kufichuka.

“Kiwembe anachukua mama na mtoto…!” watu walinong’ona.

Walinong’ona lakini haikuwa ni minong’ono iliyokuwa na mipaka maalum. Hapana. Iliyafikia masikio ya watu tofauti, na hatimaye Mama Kadala akaipata. Hakukubali kupuuzia taarifa hizo. Alimjua bintiye jinsi alivyo na mvuto mkali katika sura na umbo lake. Ni rijali gani atakayestahimili kutomtamkia neno lihusulo mapenzi endapo watakuwa na wasaa wa kuwa pamoja kwa muda mrefu?

Ndipo akaamua kufanya uchunguzi wa kina, taratibu na kwa siri kubwa. Hakutaka kumshirikisha mtu yeyote katika uchunguzi huo. Hatimaye, siku ya siku akashuhudia kwa macho, Kiwembe na Sharifa wakiwa kitandani kwake, mchana kweupe!

Alichokiona hapo, hakivumiliki wala hakisemeki. Kwanza alihisi yu ndotoni, akiota ndoto isiyopendeza. Hatimaye akazinduka na kubaini kuwa anachokishuhudia mbele yake si ndoto wala tamthiliya bali ni tukio halisi, tukio ambalo halikutofautiana na maumivu ya kisu chenye moto kikipenya kifuani mwake.

Chozi likamtoka Mama Kadala. Chozi lenye tani kadhaa za uchungu nyuma yake. Kwa ujumla hakutegemea kuwa kijana yule aliyebalehe kifuani pake, leo atokee kuwa mpenzi wa mwanae, Sharifa, wakidiriki kuchojoa nguo na kukitumia kitanda chake kwa starehe zao.

Mama Kadala alisononeka, uvumilivu ukamshinda, akaamua kupasulia ukweli Kiwembe.

“Nakuapia kijana wewe, kama hukubalehe kwenye maungo yangu haya, utaendelea kuwa kichaa wa mapenzi bila ya kudhurika. Lakini kama umebalehe hapa maungoni mwangu, halafu eti unamrudi binti yangu, wallahi nakuapia, janga litakupata katika huo wendawazimu wako.”

Wakati Mama Kadala akiongea hayo, alikwishavua nguo zote, yuko mtupu kama alivyozaliwa, machozi yakiendelea kububujika mashavuni, akimwonyesha Kiwembe kile kilichomfanya mtoto huyo akawa kichaa wa mapenzi.

Siku hiyo, saa hiyo na dakika hiyo ukawa mwisho wao wa kujuana. Kiwembe aliondoka kwa Mama Kadala kama alivyoingia. Akawa mtoto wa mitaani, mtoto asiyejali mambo ya kwenda shule wala kujitafutia riziki kwa kusaka vibarua huku na kule. Zaidi alikuwa akivizia tu kupata mlo kwa mama yake mdogo, ambaye kama kawaida yake aliendelea kutomjali.

Kwa jinsi kitongoji cha Ujiji kilivyokuwa kidogo, Kiwembe angeweza kukimaliza kimapenzi. Hata wake za watu ambao wangeingia kwenye ‘anga’ zake asingewachekea. Aliwaza mapenzi tu, na kila mwanamke mzuri aliyemtia machoni alitamani awe mpenzi wake.

Pumzi yake, mapenzi!

Shibe yake, mapenzi!

Lakini, pamoja na hayo, maneno makali ya Mama Kadala yalielea kichwani mwake bila ya kukoma, yakamfadhaisha na kumtia hofu. Akakiona kitongoji hicho kikiwa hakitofautiani na Jehanamu. Akahamia kitongoji cha Mwanga, mtaa wa Kitambwe kinyemela.


SOMA STORI KAMILI HAPA>>>>>>>>>>>>>>

Post a Comment

ads by blogger

Follow Us

Hot in week

BLOG ZINGINE

BLOG OWNER

BLOG OWNER
MESHACK JACKSON

Side Ads

Instagram

JOIN US ON TWITTER

Text Widget

Millard Ayo – Official Website

item