POLITICAL NEWS: Wabunge wa Kigoma wamtunishia misuli RC


Wabunge wa Mkoa wa Kigoma wamemtunishia misuli Mkuu wa Mkoa huo, Kanali Mstaafu Issa Machibya, kutokana na kuwatishia kuwafunga pingu kama raia wengine wa kawaida, wakisema kauli hiyo ni dharau kubwa kwao wakiwa ni moja ya mihimili mitatu ya dola wenye jukumu la kuishauri na kuisimamia serikali, hivyo anapaswa kuwaomba radhi.
Kanali Machibya anadaiwa kutoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita mbele ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, katika kongamano la uwekezaji Kanda ya Ziwa Tanganyika, mkoani Katavi, kwa kutamka kwamba, mbunge yeyote atakayekaidi maelekezo yake au maelekezo ya mkuu wa wilaya atakamatwa na kupigwa pingu kama raia wengine wa kawaida.
Wakuu wa mikoa mitatu inayounda ukanda huo, ambayo ni Kigoma, Katavi na Rukwa, walihudhuria kongamano hilo pamoja na wakuu wa wilaya na watendaji wengine, wakiwamo makatibu tawala wa mikoa (RAS)na wilaya (DAS).

MOSES MACHALI
Mbunge wa Kasulu Mjini (NCCR-Mageuzi), Moses Machali, alisema jana kuwa kwa kauli hiyo, Kanali Machibya ameonyesha kuwadharau wabunge kwamba, ni watu wasiofikiria.
“Kwa hiyo, tunamtaka ombe radhi. Aelewe kwamba, tunafanya kazi zetu kwa mujibu wa sheria. Hivyo, anapaswa aheshimu mhimili wa wabunge,” alisema Machali.

Post a Comment

1 comment

Anonymous said...

It's remarkable designed for me to have a website, which is useful for my knowledge. thanks admin
Also visit my web page transfer news liverpool

ads by blogger

Follow Us

Hot in week

BLOG ZINGINE

BLOG OWNER

BLOG OWNER
MESHACK JACKSON

Side Ads

Instagram

JOIN US ON TWITTER

Text Widget

Millard Ayo – Official Website

item