YANGA HOI KWA MTIBWA>>>> ZATOKA SARE 1-1


Vinara wa Ligi kuu soka Tanzania Bara ambao pia ni Mabingwa wa Kombe la KAGAME Yanga SC leo jumamosi Feb 02,2013  imepunguzwa kasi  baada ya kulazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Mtibwa Sugar ya Morogoro katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam .

Hadi mapumziko, Mtibwa walikuwa mbele kwa bao 1-0 lililowekwa kimiani na kiungo wa zamani wa Simba SC, Shaaban Kisiga  dakika ya 44 ya mchezo huo.
Kisiga aliyewika pia SC Villa ya Uganda na Azam FC ya Dar es Salaam alifunga bao hilo akiunganisha kwa kichwa kona maridadi ya beki Issa Rashid ‘Baba Ubaya’.
Kipindi cha pili, Kipa Hussein Sharrif ‘Cassillas’ alizuia michomo mingi ya washambuliaji wa Yanga ambao walikua wakihaha kusaka mabao, lakini Mtibwa walikuwa imara hii.
Aidha  mshambuliaji wa kimataifa wa Uganda, Hamisi Kiiza ‘Diego’ aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Didier Kabumbangu aliyeinusuru Yanga kuzama katika mchezo huo wa leo baada ya kufunga bao la kusawazisha dakika ya 86, akiunganisha pasi nzuri ya Said Bahanuzi aliyetokea benchi pia kuchukua nafasi ya Frank Domayo.

Ligi hiyo soka Vodacom Tanzania bara itaendelea hapo kesho Februari  03.02.2013. kwa Mabingwa watetezi wa kombe hilo Simba SC v  JKT Ruvu [UWANJA WA TAIFA, DSM] ili hali   Coastal Union  v Tanzania Prisons [MKWAKWANI, TANGA]
 

Matokeo hayo yanaifanya Yanga itimize pointi 33 baada ya kucheza mechi 14 na inaendelea kuongoza Ligi Kuu, ikifuatiwa na Azam yenye pointi 32, zote zimecheza mechi 14.

Related

YANGA 6057758933742857062

Post a Comment

ads by blogger

Follow Us

Hot in week

BLOG ZINGINE

BLOG OWNER

BLOG OWNER
MESHACK JACKSON

Side Ads

Instagram

JOIN US ON TWITTER

Text Widget

Millard Ayo – Official Website

item