POLITICAL NEWS: KUTOKA MKUTANO MKUU WA CCM TAIFAMakamba azima kura...

  *Kikwete apeta kwa kushindo

  *Kura zapigwa kufuata mikoa

Wajumbe mbalimbali katika upigaji wa kura
Katika kile kilichoonekana kuepusha jaribio la baadhi ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupiga kura ya maruhani dhidi ya Mwenyekiti wa Chama hicho, Rais Jakaya Kikwete,  Katibu Mkuu Mstaafu, Yusuf Makamba, jana aliuteka Mkutano Mkuu wa Chama hicho kwa kuwapiga vijembe wanachama wanaodaiwa kupanga njama hizo.

Makamba alipewa fursa ya kumnadi Rais  Kikwete kwenye mkutano huo muda mfupi kabla wajumbe kupiga kura za mwenyekiti.

Kabla ya Makamba kumnadi Rais Kikwete, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Vuai Ali Vuai, alisoma wasifu wa Kikwete kwa wajumbe wa mkutano huo.

Hatua ya Makamba kushusha vijembe ilifuatia taarifa za uvumi siku chache kabla ya kuanza kwa mkutano huo wiki iliyopita kuwa  kulikuwa na mpango wa baadhi ya wanachama kutaka kupiga kura za maruhani zenye lengo la kumpunguzia madaraka, Rais Kikwete.

Habari hizo zileleza kuwa kundi moja la wanaotaka urais wa mwaka 2015 kupitia CCM liliandaa mpango wa kumpigia Rais Kikwete kura za hapana kwa lengo la kutaka nafasi ya uenyekiti itengenishwe na urais ili kumpunguzia kazi rais.

Makamba ambaye muda wote wa hotuba yake alikuwa akinukuu vitabu vitakatifu vya Biblia na Koran, aliwaonya wanachama wa chama hicho kuepuka kupiga kura za maruhani zenye lengo la kumpunguzia madaraka Rais Kikwete.

“Umeingia kiongozi, Chama tukiwa na magari aina ya Mahndra tu, lakini leo hii kila mkoa ina Hard top halafu leo mnasema mnataka kupiga kura za maruhani ili mwenyekiti awe nani?” alihoji Makamba.

Alisema wanachama wenye nia ya kupiga kura za maruhani washindwe kwa jina la Yesu na kwamba labda atakayepiga kura ya maruhani atakuwa ni yule tu ambaye amebeba shetani mgongoni.

Hotuba ya Makamba iliwavutia wajumbe wa mkutano huo ambao walishindwa kuvumilia na kuanza kumwendea na kumtunza fedha jukwaani na hivyo kulazimika kusitisha kwa muda kuendelea kuzungumza ili kupata fursa ya kukusanya pesa hizo hali iliyozua vicheko kutoka kwa wajumbe na viongozi waliokuwa meza kuu.

Alisema Rais Kikwete ni mtu wa watu ambaye amekuwa akijitahidi kuhudhuria shughuli kadhaa ikiwamo kwenye mazishi na kutembelea wagonjwa tofauti na viongozi wengine ambao hawafanyi hivyo.

“Kuna wasaidizi wako, mtu akikupigia kura inapokelewa na mkewe anakwambia mzee amelala, lakini wewe (Kikwete) hauko hivyo unapokea simu muda wote hadi saa nane usiku,”alisema Makamba na kuongeza kuwa akiwa Katibu Mkuu wa CCM alipata tabu sana kutokana na kusema ukweli.

“Nasema hivi kwa sababu kuna watu hapa wanasema eti tumpunguzie Mwenyekiti kazi moja kwa kupiga kura za maruhani ili iwe nini?” alihoji na kuongeza:

Post a Comment

ads by blogger

Follow Us

Hot in week

BLOG ZINGINE

BLOG OWNER

BLOG OWNER
MESHACK JACKSON

Side Ads

Instagram

JOIN US ON TWITTER

Text Widget

Millard Ayo – Official Website

item