SITAISAHAU facebook


MTUNZI: Emmy John P.

MAWASILIANO: 0654 960040


SEHEMU YA KUMI NA MBILI


Nikawasha taa lakini nikahisi maumivu makali katika mikono yangu, Kheee!nikashtuka kukuta mikono yangu imevimba na ina alama ya kama michirizi hivi, hofu ikanitanda mhh!! ina maana ilikua ya kweeli ama? Kama ni kweli kwa hiyo John amempeleka wapi mama yangu? Wamempeleka wapi mwalimu Nchimbi!! Nikaendelea kutahamaki. Hali hii sasa ilikuwa ya hatari kupita zote. Gusa popote katika maisha yangu ila chunga usimguse mama yangu.

Kama hii ni kweli John lazima anieleze ni wapi wamempeleka!! Nilijiapiza.

Uwiii!!! simu yangu iko wapi nimpigie mama kama yupo salama, nilijisemesha mwenyewe huku nikiomba kisiwe kimetokea chochote kama ilivyo kwenye ndoto, nikapata simu yangu nikajaribu kumpigia hapatikani!! Nikaogopa kukubaliana na ukweli huo.

Mungu wangu mama hapatikani ana nini jamani? nilijiuliza hivyo huku nikisahau kuwa huo ulikua usiku na inawezekana akawa kazima simu..ilikua kama saa tisa za usiku..nikampigia baba naye akawa hapatikani, hofu ikanizidi nilitamani nipae nifike nyumbani nijue nini kimejili, lakini huo uwezo sikua nao..ghafla nikapitiwa na usingizi.

Bila kujua hatma ya mama!!!

Nilishtuka kutoka usingizini baada ya simu yangu kuita kwa mda mrefu, kuangalia jina ni la mdogo wangu, usingizi wote ukaniisha nikakumbuka ile ndoto ya usiku, hofu ikanitanda nikawaza au mdogo wangu alikua ananipigia kunipa habari za msiba wa mama? mara simu ikakatika.

Nikampigia mdogo wangu!!! Nijue kulikoni, wakati huo natetemeka mwili mzima. Jasho likinitoka. Sikutaka kuamini hii ndoto.

Kwa hili nilichanganyikiwa kuliko vipindi vyote nilivyowahi kuchanganyikiwa!!


*Tumepafikia sasa patamu Isabella anaapa kuwa kama John amemgusa mama yake lazima adili naye kikamilifu.

ITAENDELEA……Siri imekaribia kufichuka.

Simu ikaita. Mara ya kwanza haikupokelewa!!!
Nikazidi kutetemeka!!!
Mara ya pili simu ikapokelewa.
“Dada..shkamoo.”
Alinisalimia. Sikuweza kumjibu. Nikamuulizia mama. Akasita kunijibu. Nikamsikia akihema juu juu. Wasiwasi wangu ukazidi.
“We Helena!!” nilimuita katika simu.
“Abee!!” aliniitikia.
“Si nimekuuliza kama mama ni mzima.”
“Yeah! Ni mzima. Ila ana homa.”
“Naweza kuongea naye sasa hivi?.” Nilimuuliza hakujibu swali lile akazalisha mengine. Nikaanza kuiamini ndoto yangu!!!
“Niambie mama ana nini?” sasa nilimkaripia.
“Mama ana homa kali amelala!!.”
Nikakata simu. Nikasimama wima. Hofu kuu!!

Nifanye nini sasa!! Nilijiuliza. Kisha nikaamua kwa ujasiri kumtafuta John. Nikabonyeza namba zake. Nikawa nasikiliza huku nikitawaliwa na uoga.
Simu yake haikuwa hewani. Wasiwasi ukazidi.
Ina maana John ndio ameenda Makambako kwa mwalimu Nchimbi!! Nilijiuliza. Sikupata jawabu. Hakuwepo wa kunijibu vilevile.
Ilikuwa lazima nifanye kitu. Hapakuwa na muda wa kujilaza tena!!!
Nikaufunga mlango nikatoweka!!
Teksi niliyochukua ikanifikisha nyumbani kwa John. Nilikuwa nimeamua kuitoa siri yote ilimradi kuokoa maisha ya mama. Nilijiuliza John atanifikiriaje kwa haya mashairi ambayo naenda kumuimbia. Litakalokuwa na liwe!! Nilijitia imani.
Kama nilivyopiga simu ya John bila kupokelewa ndivyo ilivyokuwa katika mlango wake. Mlango haukufunguliwa na yeyote. Nilibaki katika mshangao hadi alipofika jirani yake na kunitaarifu kuwa hata yeye hajui John alipoenda, ni masaa kadhaa yalikuwa yamepita.
Nilikubaliana naye. Nikatoweka, moyoni nikiwa nazidi kuifuga hofu.
John hapatikani nyumbani kwake masaa yamepita, mama yangu ana homa kali. Matukio haya yanayowiana yalinitia mashaka. Mama yangu amekufa! Niliwaza huku nikiichukia hali iliyonikumba. Sikujua ni uelekeo upi natakiwa kwenda, nilisimama chini ya mti nikaanza kuwapigia simu rafiki zake John, wote wakakiri kuonana na John lakini masaa kadhaa yaliyopita. Hakuna aliyemuona muda mfupi uliopita.
“Hakuwa na safari yoyote?” Nilimuuliza mmoja wao. Akapinga hoja hiyo. Nikazidi kuumia.

Nilirejea nyumbani kwangu nikiwa nimekata tamaa sana. sikuweza kulala wakati jina la mama likinishambulia kichwa changu.
Nilijaribu mara kwa mara kupiga simu ya John. Hali ikawa ileile.

Hatimaye nikafikia maamuzi binafsi. Nikaamua kurejea Makambako nikashuhudie tatizo gani limemsibu mama yangu.
Kama ilivyokuwa awali nikazungumza tena na kiongozi wa darasa kwa ajili ya kunitetea kwa lolote litakalotokea mimi nikiwa safarini.
Nikampatia kiasi kikubwa cha pesa ili kumshawishi zaidi. Akashawishika.

Post a Comment

ads by blogger

Follow Us

Hot in week

BLOG ZINGINE

BLOG OWNER

BLOG OWNER
MESHACK JACKSON

Side Ads

Instagram

JOIN US ON TWITTER

Text Widget

Millard Ayo – Official Website

item