ESCAPE FROM SOBIBO ATOROKA GEREZANI la ZUBERI na KUVUA NGUO ASIKAMATWE

Na Nassor Wazambi (facebook)


Mwananchi mmoja kwa kushirikiana na askari wa kikosi cha kuzuia ghasia FFU mjini Tabora wamefanikiwa kumkamata mfungwa mmoja wa gereza la mahabusu Tabora wakati akifanya jaribio la kutoroka akiwa amevua nguo na kubakia uchi wa mnyama.
Mfungwa huyo ambaye anafahamika kwa jina la Jonas Oscar(25)imedaiwa kuwa mnamo majira ya mchana siku ya tarehe 14 januari 2013 alifanya jaribio hilo wakati akiwa kwenye kazi za bustanini na wafungwa wenzake.
Hata hivyo wakati akiwa ameanza safari hiyo ya kukwepa kifungo cha mwaka mmoja ambacho ameanza kukitumikia mapema mwaka huu,mfungwa huyo Jonas aliibukia katika kambi ya Jeshi la Polisi iliyoko jirani na gereza hilo la mahabusu hatua ambayo ilisababisha kuonwa mapema kwakuwa alionekana kuwa ni mtu wa ajabu kwa kukimbia akiwa uchi wa mnyama.
Aidha katika hatua nyingine mfungwa huyo amefikishwa mahakama ya wilaya ya Tabora,mbele ya hakimu Mheshimiwa Magori na kukabiliwa kwa kosa la kutoroka chini ya ulinzi halali kinyume cha sheria namba 16 kifungu cha 116 ya mwaka 2002,ambapo alihukumiwa kutumikia adhabu kwenda jela kwa kifungo cha miezi 16,adhabu ambayo ameanza kuitumikia mara moja.
Awali Jonas Oscar imedaiwa kuwa alikuwa akitumikia kifungo cha mwaka mmoja akiwa ni mfungwa No.02,2013 katika Gereza la mahabusu Tabora mjini baada ya kupatikana na hatia ya kutishia kumuua baba yake mdogo huko katika wilaya ya Sikonge mkoani Tabora.

Mwananchi mmoja kwa kushirikiana na askari wa kikosi cha kuzuia ghasia FFU mjini Tabora wamefanikiwa kumkamata mfungwa mmoja wa gereza la mahabusu Tabora wakati akifanya jaribio la kutoroka akiwa amevua nguo na kubakia uchi wa mnyama.
Mfungwa huyo ambaye anafahamika kwa jina la Jonas Oscar(25)imedaiwa kuwa mnamo majira ya mchana siku ya tarehe 14 januari 2013 alifanya jaribio hilo wakati akiwa kwenye kazi za bustanini na wafungwa wenzake.
Hata hivyo wakati akiwa ameanza safari hiyo ya kukwepa kifungo cha mwaka mmoja ambacho ameanza kukitumikia mapema mwaka huu,mfungwa huyo Jonas aliibukia katika kambi ya Jeshi la Polisi iliyoko jirani na gereza hilo la mahabusu hatua ambayo ilisababisha kuonwa mapema kwakuwa alionekana kuwa ni mtu wa ajabu kwa kukimbia akiwa uchi wa mnyama.
Aidha katika hatua nyingine mfungwa huyo amefikishwa mahakama ya wilaya ya Tabora,mbele ya hakimu Mheshimiwa Magori na kukabiliwa kwa kosa la kutoroka chini ya ulinzi halali kinyume cha sheria namba 16 kifungu cha 116 ya mwaka 2002,ambapo alihukumiwa kutumikia adhabu kwenda jela kwa kifungo cha miezi 16,adhabu ambayo ameanza kuitumikia mara moja.
Awali Jonas Oscar imedaiwa kuwa alikuwa akitumikia kifungo cha mwaka mmoja akiwa ni mfungwa No.02,2013 katika Gereza la mahabusu Tabora mjini baada ya kupatikana na hatia ya kutishia kumuua baba yake mdogo huko katika wilaya ya Sikonge mkoani Tabora.


Related

POLICE 3176573969562980138

Post a Comment

ads by blogger

Follow Us

Hot in week

BLOG ZINGINE

BLOG OWNER

BLOG OWNER
MESHACK JACKSON

Side Ads

Instagram

JOIN US ON TWITTER

Text Widget

Millard Ayo – Official Website

item