FACEBOOK CHATTING============== 5

 MWANDISHI: NYEMO CHILONGANI.

MAHALI: DAR ES SALAAM.

SIMU: 0718 069 269




MSICHANA: Ndio najiandaa mpenzi. Unataka nivae mavazi gani?
MIMI: Vyovyote tu. Ila sipendelei kukuona ukivaa suruali.
MSICHANA: Kwa nini?
MIMI: Sina sababu.
MSICHANA: Basi usijali. Nitavaa gauni moja zuri sana ambazlo nilinunuliwa na baba katika moja ya maduka makubwa jijini New York. Nitakuja nalo huko.
MIMI: Poa. Wewe njoo tu mpenzi.
MSICHANA: Ili uwahi, naomba ufanye kitu kimoja.
MIMI: Kipi?
MSICHANA: Kodi bajaji na hela nitalipia mimi huku.
MIMI: Poa. Ila usiniingize choo cha kike.
MSICHANA: Usijali mpenzi.

Nikaanza kujiandaa kwa haraka sana, japokuwa toka nizaliwe sikuwahi kufika mapema sehemu ya appointment ila siku hiyo nilitaka kufika mapema sana. Nilipomaliza kujiandaa, nikaanza kwenda kwenye maegesho ya madereva wa mabajaji ambako nikamuita rafiki yangu ambaye alikuwa akiendesha bajaji moja.

MIMI: Sikiliza Moody, nataka unipeleke Slipway. Kiasi gani?
MOODY: Du! Unakwenda kufanya nini tena?
MIMI: Achana na hayo. Kiasi gani?
MOODY: Elfu kumi.
MIMI: Poa. Ila naomba tufanye kitu kimoja.
MOODY: Kitu gani?

Related

HADITHI 7045503866002733056

Post a Comment

ads by blogger

Follow Us

Hot in week

BLOG ZINGINE

BLOG OWNER

BLOG OWNER
MESHACK JACKSON

Side Ads

Instagram

JOIN US ON TWITTER

Text Widget

Millard Ayo – Official Website

item