RIWAYA: WASALIMIE KUZIMU---2

MTUNZI: Hussein Wamaywa

SIMU: 0755 697335


... Ni ile mikono yenye nguvu iliyokuwa imembana kiunoni kwa nguvu ndiyo iliyomshitua na kumuondoa toka katika njozi hiyo tamu aliyokuwa akiiota, alipogeuka nyuma akakuta jamaa linataka kumbaka.
Halfan akakurupuka baada ya kuhisi nini kinataka kuendelea hata hivyo juhudi zake za kutaka kujinasua zilikwama baada ya kujikuta amedhibitiwa vizuri na jamaa yule.Hakutaka kukubali kirahisi akakunja mkono upesi na kuachia kipepsi kilichotua sawia shingoni mwa jamaa. Akainuka na kuliacha likigugumia kwa maumivu.
Akashukuru Mungu na kuona kwamba njemba lile lilikuwa halijafanikiwa kutimiza lengo lake. Macho yake yalipozoea giza ndipo alipotambua kwamba aliyetaka kumbaka hakuwa mwingine zaidi ya Jofu Gideon.
Mbele yake aliwashuhudia wababe wengine watatu wakiwanajisi vijana wengine wawili ambao hawakuwa na muda mrefu toka walipoongezwa katika chumba hicho. Ilikuwa picha isiyopendeza ambayo alilazimishwa kuitazama.
Hakulala tena! Badala yake akakaa pembeni na kuitafakari ndoto aliyokuwa akiiota ambayo tayari ishamfanya aichafue Kaptura yake.
Jina Shania halikuwa kabisa katika kumbukumbu zake. Alijitahidi kumkumbuka na kumtafuta tena na tena kati ya wanawake wengi aliokwisha rusha nao roho, wasichana wa shule, mabaamedi, wanamitindo, makarani, warembo na hata mabosi!
Bado jina Shania halikuingia katika reli zake.
Aliposhindwa kabisa akaachana nae na kuyafiria maneno ya Shania, kiasi yalikuwa na ukweli ndani yake. Ni kweli Nasra hajawahi kuja walau kumpa hata pole, wachilia mbali kumjulia hali.
Hakuwa Nasra pekee tu bali hata marafiki zake wengine waliokuwa nae sambamba wakati akiwa uraiani. Sasa ndio akagundua ni kwa nini marafiki wanaitwa wanafiki, aliamini yeye sio mtu wa kupata dhiki ya vitu vidogo vidogo kama maji, sabuni nyembe, mafuta na hata sigara.
Hivi vilikuwa vitu vidogo sana ambavyo marafiki zake wengeweza kumsaidia pasipo kupata hasara yeyote. Lakini wachilia mbali kumpelekea vitu hivyo wameshindwa kwenda hata kumuona.
Ni wakati huo alipopambazukiwa na ukweli kwamba ni kwa nini wahenga walisema rafiki wa kweli hupatikana wakati wa shida. Aliendelea kuwaza hili na lie na kumlaumu huyu na yule mpaka kulipokucha.
Naam! Alikuwa ameingia katika mkondo wa maisha mapya kwa kosa la kipumbavu kabisa na ndio maana wafungwa na gereza walimdharau yeye na kosa lake…
ENDELEA HAPA>>>>>>>>>

Related

HADITHI 4787484323358166745

Post a Comment

ads by blogger

Follow Us

Hot in week

BLOG ZINGINE

BLOG OWNER

BLOG OWNER
MESHACK JACKSON

Side Ads

Instagram

JOIN US ON TWITTER

Text Widget

Millard Ayo – Official Website

item