SITAISAHAU facebook-----------------23

MTUNZI: Emmy John P.

MAWASILIANO: 0654 960040

SEHEMU YA ISHIRINI NA TATU

...
Nikafadhaishwa baada ya yule Davis ambaye sasa niliamini naenda kummalizia alipogeuka kuwa joka kubwa la kijania. Haraka nikawahi kujitoa lakini nilikuwa nimechelewa sana. Joka lile likawahi kujiviringisha kuanzia kiunoni likawa linapanda juu. Sasa lilikuwa limenifunga hadi kifuani.
Ajabu!! Lilikuwa linawasha sana.nilitamani kujikuna lakini haikuwezekana na mikono ilikuwa imefungwa tayari.
Nililiamuru liniachie lakini halikuiheshimu amri yangu. Nikazidi kuwashwa, nikajaribu kujigalagaza, haikuwezekana. Sasa likaanza kujikaza, muwasho ukaenda likizo, maumivu yakaingia kati. Lilizidi kukaza, mara likaongeza kujiviringisha hadi likaniziba usoni. Kifo kikanukia harufu ya kukera.
Nikabaki jicho moja tu kuona nje!! Viungo vingine vyote vilikuwa vimefunikwa. Sikuwa na ujanja. Jicho langu likamuona John akiwa ameshangaa kama tahira. Nilijaribu kutoa sauti haikutoka, nilikuwa namwomba John kwa mara ya mwisho aweze kuniokoa. Hakuweza kunisikia.
Nikatazama juu nikakutana na mawingu yenye rangi inayoshabihiana na buluu, nikaikumbuka rangi ya mtandao wa kijamii. Ni huku nilikutana na Dokta Davis. Akanipa zawadi ya utajiri, akanipatia kazi nyepesi inayonipatia kipato kikubwa. Nikamuamini sana. Sasa alikuwa amegeuka joka kubwa na lilikuwa linaniua.
Hakika lazima nife!! Jitihada zangu zote hazikuwa na maana tena.
John hakuwa msaada wowote kwangu. Na hakuwepo mwingine wa kunipa msaada.
Nilipofikiria ni nani mwingine wa kunisaidia akili yangu ikaejea kwa mwalimu Nchimbi. Mama yangu mzazi. Nikajaribu kuita sauti haikutoka. Mama naye hakuwa na msaada katika hali hii.
Nikayakumbuka maneno ya mama. Miaka mingi sana nikiwa mdogo aliwahi kunikambia maneno.
“Yupo mtu anakusikia hata usipotoa sauti.” Hili lilikuwa jibu alilonipa baada ya kumuuliza iwapo mabubu na viziwi wanaweza kuzungumza na Mungu. Jibu lake hadi ukubwani halikunitoka.
Nami sasa nilikuwa bubu. Jaribio la mwisho kabisa ni kuzungumza na yule anayesikia wakati wote. Ajuaye unachokiwaza. Kila wakati, mahali popote.
Mungu!

SASA ENDELEA KUSOMA HAPA>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>

Related

HADITHI 8210074981845020788

Post a Comment

ads by blogger

Follow Us

Hot in week

BLOG ZINGINE

BLOG OWNER

BLOG OWNER
MESHACK JACKSON

Side Ads

Instagram

JOIN US ON TWITTER

Text Widget

Millard Ayo – Official Website

item