SITAISAHAU facebook------------------25

MTUNZI: Emmy John p.


MAWASILIANO: 0654 960040

SEHEMU YA ISHIRINI NA TANO

...
Maskini yule dada bila kujua kwamba ameambiwa anipatie kinga. Akadhani yule mbongo amemaanisha ule mkoba. Akaniomba msamaha kwa kila namna kisha kwa ukarimu kabisa akanipatia ule mkoba. Ulikuwa mzito kiasi. Nilipotaka kuondoka yule dada aliyekuwa amejikita katika kutafuta anachojua yeye, aliniita, nikageuka na kumshangaa kidogo.
“Unatakiwa kuweka sahihi.” Alinielezea kwa ukarimu.
Nikaona kama huyu binti ana nia mbaya na mimi. Nikabaki wima najiuliza iwapo niende mbele ama nirudi. Tukatazamana kwa sekunde kadhaa. Nikaona isiwe tabu. Nikarejea nikachukua kalamu niweze kuweka sahihi. Mara nikasikia fujo za mlango kufunguliwa.
Nikaomba Mungu usiwe mlango wa yule jamaa mbongo. Kisha nikasikia hatua kubwa kubwa zikitambaa.
“How long does it take to…to…..hell..” (Inachukua muda gani ku…ku…. ). Ilisikika sauti yenye kitetemeshi cha hasira. Alikuwa yule mbongo.
Sasa badala ya kuweka sahihi nikabaki kulishikashika tu lile daftari na kalamu. Mkojo ukatoka safari yange ya mbali na sasa ulikuwa unahitaji kutoka. Nikabana miguu yangu!! Mkoba mkononi.
Ninafumaniwa Isabela mimi!!
Nikataka nikimbie!! Miguu ikawa mizito. Sikuwahi kufanya kitendo cha wizi hivyo lazima hali kama hii ingenitokea.
“Iam sorry boss..i have already given her (samahani mkuu..nimempatia tayari.)” yule dada wa mapokezi alijitetea kwa uoga. Mara vile vishindo vikasita.
Yakafululiza matusi ya nguoni kutoka kwa yule mlevi wa kibongo.
Hapo sasa nikaangusha saini yangu.
Narudi vipi na ule mkoba sasa!! Nikajikaza nikaanza kuondoka.
Nilipogeuka nikakutana na kosa ambalo nililitegemea. Yule dada wa mapokezi alikuwa amebonyea chini tena.
Asante! Nilimshukuru kwa kitendo hicho.
Ghafla nikabadili uelekeo. Nikaelekea katika vyoo.
Upande huu, nikaambaa na korido hadi nikaufikia mlango wa kutokea. Nikamuachia tabasamu mlinzi aliyekua kwa nje na yeye akatabasamu. Tabasamuu la kizee. Kisha nikatoweka. Nikapiga hatua kwa hatua hadi nikalifikia geti kuu la kutokea. Hapa nilitakiwa kuandika jina. Nikaandika jina lililokuja kichwani mwangu lakini sio jina sahihi.
Geti likafunguliwa. Mimi na mkoba wangu. Nikatoka.
Nilipogeuka nyuma nikakutana na maneno mazuri ya kupendeza.

The Savoy Hotel
12 Buteko Avenue
Ndola
Zambia

Haya hayakuwa yananihusu. Niligeuka na kutazama mbele. Nikaanza kutokomea. Nikashtuliwa kwa kuguswa begani.
Nikageuka upesi nikaikuta amani ambayo nilikuwa naihitaji.
Samson…jemedari wa kisukuma.
Akanikumbatia kunipongeza. Lile joto lake likanikumbusha mengi. Nikapuuzia.

Oparesheni ilikuwa imekamilika.
SASA ENDELEA>>>>>>>>>>>>

Related

HADITHI 6277116696948602749

Post a Comment

ads by blogger

Follow Us

Hot in week

BLOG ZINGINE

BLOG OWNER

BLOG OWNER
MESHACK JACKSON

Side Ads

Instagram

JOIN US ON TWITTER

Text Widget

Millard Ayo – Official Website

item