BBC:Wafaransa wapinga ndoa ya jinsia moja

Maandamano mjini Paris kupinga ndoa za jinsia moja
Maelfu ya Wafaransa wameandamana katika barabara za mjini Paris kupinga mpango wa serikali kuhalalisha ndoa kati ya jinsia moja.
Mswada uliopendekezwa na serikali ya kisoshalisti ya Francois Hoillande itaruhusu watu wa jinsia moja kuoana na kulea watoto.
Watu kama laki moja wameandamana katika mihadhara mitatu tofauti na kukusanyika karibu na Eiffel Tower.
Waliotayarisha maandamano hayo wanasema waliohudhuria ni nusu milioni.
Watu walitoka sehemu mbali-mbali za nchi kwa mabasi maalumu yaliyokodiwa pamoja na treni kwa sababu wanaona mpango wa serikali kuhalalisha ndoa kati ya watu wa jinsia moja na kulea watoto, utaharibu msingi muhimu wa jamii.
Bunge linatarajiwa kujadili mswada huo baadae mwezi huu.
Maandamano yanaungwa mkono na kanisa la Katoliki na upande wa upinzani wa mrengo wa kulia.
Lakini wasemaji wanashikilia kuwa maandamano hayo siyo ya kisiasa wala ya kidini na wala hayawalengi wapenzi ya jinsia moja.
Maandamano hayo ni upinzani mkubwa kabisa dhidi ya Rais Hollande tangu kuingia madarakani mwezi wa May.

Related

UFARANSA 4875150013284107996

Post a Comment

ads by blogger

Follow Us

Hot in week

BLOG ZINGINE

BLOG OWNER

BLOG OWNER
MESHACK JACKSON

Side Ads

Instagram

JOIN US ON TWITTER

Text Widget

Millard Ayo – Official Website

item