BBC:Ajali ya treni yawajeruhi 100 Afrika KUSINI

Afrika Kusini
Afrika Kusini
Magari ya moshi mawili yamegongana nchini Afrika Kusini karibu na mji mkuu wa Pretoria. Takriban watu 100 walijeruhiwa.
Wauguzi walisema kwamba watu 20 walijeruhiwa vibaya katika ajali hiyo.
"Magari ya moshi yote mawili yalikuwa yamejaa wasafiri ambao husafiri kwenda Pretoria kila siku , wakiwemo watoto wengi tu waliokuwa wanaelekea shuleni," msemaji wa huduma za dharura aliliambia shirika la habari la AFP.
Afrika Kusini inakarabati mtandao wake wa safari za gari moshi ambao umezeeka.
Ajali hiyo ilitokea mapema asubuhi baada ya gari moshi mmoja lilipogongana na lingine lililokuwa limeegeshwa karibi na Attridgeville, kamji kadogo magharibi mwa Pretoria.

CHANZO BBC SWAHILI

Related

TRENI 8035203124137319446

Post a Comment

ads by blogger

Follow Us

Hot in week

BLOG ZINGINE

BLOG OWNER

BLOG OWNER
MESHACK JACKSON

Side Ads

Instagram

JOIN US ON TWITTER

Text Widget

Millard Ayo – Official Website

item