Mshiriki Maisha Plus afariki dunia

ALIYEKUWA mshiriki wa shindano la Maisha Plus 2012, Rashid Ndunduke, amefariki dunia kijijini kwao juzi baada ya kuvamiwa na kiboko.

 Rashid ambaye kwenye shindano hilo la Maisha Plus alikuwa akiwakilisha Mkoa wa Lindi, alikuwa kivutio kwa watazamaji wengi, hasa kwa mambo mbalimbali aliyokuwa akifanya ndani ya kijiji hicho, ikiwamo kuonesha maisha halisia.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na kaka wa marehemu, Hassan Ndunduke, mdogo wake alikutwa na mauti akiwa anavua samaki, ghafla kiboko alimvamia na kumjeruhi.
Hassan alisema licha ya juhudi za hospitali ya jirani huko kijijini kwao Njinjo kuokoa maisha yake zilishindikana.
Marehemu alijiunga Maisha Plus kama mmoja wa wawakilishi wa Mkoa wa LindiAkiwa kijijini Maisha Plus, alifahamika kwa wengi kama Nanjilinji, Master Key au Baba Sampo.
Shughuli alizozifanya Maisha Plus ni pamoja na kuuza duka, uchongaji na kuna wakati aliwahi kuongoza kwa kuwa na fedha nyingi zaidi ikilinganishwa na wanakijiji wenzake, sambamba na uhodari wa kukwea miti mirefu

Related

VIFO 2858395938391276638

Post a Comment

ads by blogger

Follow Us

Hot in week

BLOG ZINGINE

BLOG OWNER

BLOG OWNER
MESHACK JACKSON

Side Ads

Instagram

JOIN US ON TWITTER

Text Widget

Millard Ayo – Official Website

item