KUMBUKUMBU YA MWAKA MMOJA TANGU KUFARIKI MSANII STEVEN KANUMBA

Mama Mzazi wa Steven Kanumba, Flora Mtegoa akilia juu ya kaburi la mwanae, November 2012
Steven Kanumba akiwa katika ofisi za Global Publishers baada ya kurudi kutoka Afrika Kusini katika jumba la BBA Septemba 11, 2009.
...Akiwa na Mhariri Mtendaji wa Global Publishers, Richard Manyota.
Kanumba akihojiwa na Sauda Mwilima (kushoto) alipokwenda kutoa msaada katika kituo cha watoto yatima  cha  CHAKUWAMA kilichopo Sinza jijini Dar es Salaam, Agosti 2011.
Steven Kanumba akiwa na furaha baada ya kupokelewa Uwanja wa Ndege akitokea nchini Afrika Kusini alipokuwa amealikwa kama staa katika jumba la BBA Septema 9, 2012.
Kanumba akisalimiana na Mzee Kipara alipomtembelea nyumbani kwake Kigamboni, Septemba 2010. Wasanii wote wawili kwa sasa ni marehemu.
Staa wa filamu kutoka Nigeria, Ramsey Noah, akiongea na wanahabari baada ya kuwasili nchini kushiriki katika filamu iliyopewa jina la Devil’s Kingdom ambayo iliandaliwa na Kanumba (pembeni), Aprili 2011.
Steven Kanumba (kulia) akibadilishana mawazo na Mkurugenzi wa Paradise Hotel Justuce Bagumu (kushoto)  na Ramsey Tokumbo Nouah (katikati) ndani ya ukumbi wa Paradise Hotel wakati wa hafla ya kumuaga Ramsey baada ya kukamilisha filamu ya Devil's Kingdom, iliyoandaliwa na kampuni ya Kanumba The Great Films Production Aprili 2011.
Ujumbe uliopo katika kaburi la Kanumba.
LEO ni mwaka tangu msanii maarufu wa filamu Bongo, Steven Charles Kanumba kuiaga dunia. Marehemu Kanumba alifariki dunia alfajiri ya Jumamosi Aprili 7, 2012 akiwa na umri wa miaka 28, baada ya kile kilichodaiwa kuwa ni ugomvi wa kimapenzi na rafiki yake wa kike, Elizabeth Michael kwa jina maarufu “Lulu” na kuzikwa Aprili 10, 2012 na maelfu ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam na wengineo.
Mpaka sasa bado hajatokea msanii wa kuziba pengo aliloliacha marehemu katika tasnia ya filamu. Pichani juu ni baadhi ya taswira za marehemu enzi za uhai wake zilizochukuliwa na mtandao huu.
Mungu ailaze roho ya marehemu Steven Charles Kanumba mahali pema peponi.

Related

KANUMBA 183818577008347464

Post a Comment

ads by blogger

Follow Us

Hot in week

BLOG ZINGINE

BLOG OWNER

BLOG OWNER
MESHACK JACKSON

Side Ads

Instagram

JOIN US ON TWITTER

Text Widget

Millard Ayo – Official Website

item