RIWAYA: MREMBO ALIYEPOTEA---------- 3

MTUNZI: Andrew Carlos

MAWASILIANO: 0713133633

SEHEMU YA TATU

...
Alice aliita kwa sauti ya uoga uoga huku akijiumauma kwa kutokujiamini bila majibu yeyote kwani ndio kwanza Angel alijigeuza na kuendelea kuuchapa usingizi. Uzalendo ukamshinda baada ya kuona Angel hashtuki wala kuamka. Alichokifanya akaufungua mlango taratibu huku akinyata nakutoka nje.
“Samahani, eti uani wapi?”
Sasa Alice akawa amekutana uso kwa uso na jirani mmojawapo. Yule jirani akamsikiliza na kumwangalia Alice kwa jicho la dharau kisha akamfyoza na kuendelea na shughuli zake bila kumjibu chochote. Alice akajiskia mwenye bahati mbaya na watu lakini akajikaza moyo na kuendelea kuangaza kila pande hadi alipofanikiwa kuuona mlango wa choo. Kitendo cha yeye kuongoza mpaka chooni na kisha kuvua nguo haraka haraka. Ule mkojo uliokuwa unamsumbua sasa ukawa haupo tena kwake kwani ulishaijaza nguo yake ya ndani, ikawa imelowa tepetepe. Alice akaogopa sana kutoka chooni akiwa amelowa katika nguo yake ya ndani, woga ukazidi kutanda na hakuwa na jinsi zaidi ya kuendelea kukaa chooni huku akitafakari ni jinsi gani ataweza kurudi chumbani akiwa amelowa nguo yake ya ndani tepe tepe.
“Alice?, Alice mdogo wangu upo chooni?”
Sauti ya Angel tayari ilikuwa nje ya choo ikimtafuta Alice na sasa alikuwa nje ya kile choo akigonga ili Alice atoke.
Woga ukawa bado umemtanda Alice. Mwili wote ukawa ukiendelea kumtetemeka, mapigo yake ya moyo yakaanza safari ya kwenda kasi mithili ya gari liliopo katika mteremko mkali. Akaiangalia ile nguo yake ya ndani kwa hasira huku akijuta kitendo cha yeye kuchelewa kuwahi chooni.
“Abee dada!! , nipo huku chooni!”
“Aanhaa!!, nilishtuka mdogo wangu nilidhani umeondoka

ENDELEA KUSOMA HADITHI HII>>>>>>>>>>>>>>

Related

HADITHI 5954275511022918262

Post a Comment

ads by blogger

Follow Us

Hot in week

BLOG ZINGINE

BLOG OWNER

BLOG OWNER
MESHACK JACKSON

Side Ads

Instagram

JOIN US ON TWITTER

Text Widget

Millard Ayo – Official Website

item