RIWAYA: MREMBO ALIYEPOTEA-----------------5

MTUNZI: Andrew Carlos

MAWASILIANO: 0713133633

SEHEMU YA TANO


Ule mkojo uliokuwa ukimchuruzika John kidogo kupitia suruali yake kwa uoga sasa ukawa umeongeza kasi nakuwa mwingi sana hali iliyofanya suruali yake yote kulowana na lile kojo. Alijikaza kiume na kisha akamnyanyua Angel kwa kumbeba mithili ya wacheza mieleka kisha akaongoza mpaka kwenye gari lake nje nakumuhifadhi halafu akarudi tena ndani kumchukuwa Alice naye akampakazia kwenye gari lake nakuelekea hospitali ya Amana.
“Mungu nisidie nifike salama, Eeeh Baba niongoze ningoze Baba” OOohhh!!”
Barabara haikuwa na foleni kabisa sababu ilikuwa ni usiku sana, gari zilikuwa chache sana alizokuwa akipishana nazo John, njia nzima alikuwa akimuomba Mungu afike salama. Japo mikono yake ilikuwa ikimtetemeka lakini alijitahidi kujikaza kiume mpaka akafanikiwa kuingia katika hospitali ya Amana kisha akaomba msaada pale mule ndani.
“Umesema umekuja na maiti au mgonjwa”
“Mimi nahisi watakuwa wote wagonjwa maana nahisi kama wamezi mia kwani huyu mmoja alizinduka baada ya kumpepea sana akazimia tena ila huyu mwingine sikumuona akizunduka”
John alikuwa akiongea na daktari wa zamu ambaye kwa muda huu alikuwa karibu na ile miili ya Alice na Angel kwenye wodi ya wagojwa mahututi akiikagua vizuri.
“Umesema walipatwa na nini?”
“Hapana Dokta wala sijui mie nilikuwa ofisini sasa nimerudi nakuta wote wamezimia..”
“Hawa ni kama nani kwako?”
“Huyu hapa mmoja ni mke wangu anaitwa Angel na huyu ni mdogo wake anaitwa Alice wote wanaishi pamoja”
Dakatri alichukuwa vipimo vyake kwa kuwapima mapigo ya moyo kisha akaingiza mkono wake mifukoni na kutoa tochi za kupimia wagonjwa waliokufa halafu akafungua macho ya Alice na kummulika.

ENDELEA KUSOMA HAPA>>>>>>>>>>>>>>>>

Related

HADITHI 7725145347038310300

Post a Comment

ads by blogger

Follow Us

Hot in week

BLOG ZINGINE

BLOG OWNER

BLOG OWNER
MESHACK JACKSON

Side Ads

Instagram

JOIN US ON TWITTER

Text Widget

Millard Ayo – Official Website

item