RIWAYA: PAINFUL TRUTH (UKWELI WENYE KUUMA)------------------- 1


MTUNZI: Nyemo Chilongani

MAWASILIANO: 0718 06 92 69

SEHEMU YA KWANZA


Msichana Happy alikuwa akilalamikia uchungu ambao ulikuwa umemshika katika kipindi ambacho alikuwa shambani akilima. Damu zikaanza kumtoka katika sehemu zake za siri, akalitupa jembe lake pembeni na kuanza kulishika tumbo lake ambalo aliliona kuwa katika maumivu makali.
Mama yake ambaye alikuwa pembeni pamoja na wakulima wengine wakaanza kumsogelea, Happy alionekana kuhitaji msaada kwa wakati huo. Wakatandika kanga zao chini na kisha kuanza kumzalisha pale pale shambani. Mpaka wanafanikiwa kumtoa mtoto, Happy alikuwa amepoteza damu nyingi sana mwilini mwake.
Mtoto mchanga alikuwa akilia, walipomwangalia vizuri, waligundua kwamba alikuwa mtoto wa kiume. Walichokifanya ni kumuinua Happy na kisha kumpeleka katika kivuli cha mti wa mwembe ambao ulikuwa pembeni kidogo ya shamba hilo.
Happy bado alikuwa akiendelea kulia, maumivu makali bado yalikuwa yamelikamata tumbo lake. Kwa haraka haraka mzee Lyimo akachukua baiskeli yake aliyokuwa ameiegesha pembeni na kisha kumpakiza Happy na safari ya kuelekea katika zahanati ya Machame kuanza.
Njia nzima Happy alikuwa akilia, maumivu yalikuwa yakiongezeka kadri muda ulivyozidi kwenda mbele. Mpaka wanafika Zahanati, Happy alikuwa hoi, hakuwa akiweza hata kusogeza kiungo chake chochote cha mwili wake.
Manesi ambao walikuwa nje wakipiga stori, wakaanza kuwasogelea, wakamteremsha Happy kutoka katika baiskeli ile na kisha kuelekea ndani ya Zahanati hiyo. Mama yake Happy, Vanessa alikuwa amembeba mjukuu wake huku akijitahidi kumbembeleza aache kulia.
Happy akaingizwa ndani ya moja ya chumba cha zahanati ile na kisha kulazwa kitandani. Bado alikuwa akiendelea kulia kutokana na maumivu makali ambayo alikuwa akiyasikia yakizidi kadri muda ulivyozidi kwenda mbele. Manesi wakaanza kumhudumia Happy mpaka pale ambapo dokta wa zahanati ile alipofika.
Mzee Lyimo na mkewe, Bi Vanessa walikuwa nje wakisubiri kusikilizia ni kitu gani ambacho kilikuwa kimeendelea ndani ya chumba kile. Wala hazikupita dakika nyingi, dokta akatokea mahali pale. Akaanza kuwaangalia huku macho yake yakionyesha wasiwasi fulani, aliporidhika, akaiweka vizuri miwani yake.
“Mtoto wake yupo wapi?” Dokta aliuliza.
ENDELEA KUSOMA HAPA>>>>>>>>>>>>>

Related

HADITHI 786883205389364986

Post a Comment

ads by blogger

Follow Us

Hot in week

BLOG ZINGINE

BLOG OWNER

BLOG OWNER
MESHACK JACKSON

Side Ads

Instagram

JOIN US ON TWITTER

Text Widget

Millard Ayo – Official Website

item