MWANASPOTI::::KOPUNOVIC AIBADILISHA SIMBA SASA INA KASI, NGUVU


SIMBA imebadilika kidogo na sasa Kocha mpya Goran Kopunovic anataka wachezaji wake wacheze soka la kasi huku wakizuia kwa umakini mkubwa kwa dakika zote 90 za mchezo.
Katika siku yake ya kwanza kwenye mazoezi ya timu hiyo jana Ijumaa Kwenye Uwanja wa Ngome uliopo Fuoni, Kopunovic raia wa Serbia aliyechukua nafasi ya Patrick Phiri wa Zambia, alitumia muda wa dakika 90 kuanzia saa 10:00 hadi saa 11:30 jioni katika mazoezi, kisha akafanya mkutano mdogo na wachezaji wake.
Kocha huyo aliwaelekeza wachezaji wake kufanya mazoezi ya kukimbia kwa dakika 30 ili kutengeneza pumzi na stamina na kisha akawasimamisha na kuwapa zoezi la kumiliki mpira huku wakikokota jambo lililoonekana kupokelewa vizuri na wachezaji wake.
Baada ya mazoezi hayo Kopunovic alisema; “Najua wachezaji wana mawazo ya kupoteza mechi ya kwanza, nimewataka wasahau matokeo ya mechi hiyo kwani sasa tunajenga timu. Nataka wacheze soka la kasi na pasi za haraka lakini viungo wakabe wasiruhusu wapinzani kupenya katika eneo lao.
“Nataka kuirudishia timu uwezo wa kupambana kwa dakika 90 kwani kwenye mechi yao na Mtibwa walicheza kwa dakika 30 tu kisha wakapotea, ndiyo maana nimewafanyisha mazoezi ya kuongeza pumzi,” alisema Kopunovic
Kocha huyo alisisitiza kwamba ili Simba iweze kupata matokeo mazuri uwanjani ni lazima icheze soka la kasi, nguvu na wachezaji wake wapambane kwa dakika 90 vinginevyo itaendelea kupata matokeo yasiyoridhisha.
Simba imepoteza mechi mbili ndani ya wiki moja kwani Desemba 26, mwaka jana ilifungwa bao 1-0 na Kagera Sugar katika Ligi Kuu Bara halafu ikapoteza mchezo juzi Alhamisi dhidi ya Mtibwa kwa bao 1-0 ikiwa ni mechi yao ya kwanza ya Kombe la Mapinduzi.
Wakati huohuo, Kopunovic ametangaza hali ya hatari kwa wachezaji wa kigeni wa Simba ambao hawapo kikosini kwa ruhusa au matatizo ambayo hayafahamiki na uongozi wakiwemo Juuko Murshid, Simon Sserunkuma, Joseph Owino, Emmanuel Okwi na Joseph Owino wote raia wa Uganda.
“Lazima timu iwe na nidhamu haiwezekani wachezaji wote wanne wa kigeni wasiwepo na timu hapa, wao wanatakiwa kuwa tofauti na wenzao wazawa. Nimeuambia uongozi nawahitaji na lazima waje,” alisema Kopunovic.

Related

Sports 6671865847972580960

Post a Comment

ads by blogger

Follow Us

Hot in week

BLOG ZINGINE

BLOG OWNER

BLOG OWNER
MESHACK JACKSON

Side Ads

Instagram

JOIN US ON TWITTER

Text Widget

Millard Ayo – Official Website

item