FACEBOOK CHATTING--------- 3



MWANDISHI: NYEMO CHILONGANI.

MAHALI: DAR ES SALAAM.

SIMU: 0718 069 269



MSICHANA: Mbona kimya?
MIMI: Unajua internet connection inazingua sana. Yaani mara ikate, mara irudi. Yaani tabu tupu.
MSICHANA: Poleee. Naomba unijibu basi.
MIMI: Ninae kwa sasa.
MSICHANA: Unae?
MIMI: Ndio. Ila hanionyeshei mapenzi ya dhati. Mara nyingi najitahidi kumtumia meseji, hanijibu, nikimpigia simu usiku, ipo bize tu. Tena si hivyo tu, hadi usiku wa manane ipo bize. Unahisi nini hapo?
MSICHANA: Unaibiwa.
MIMI: Kama naibiwa, nawe upo tayari kumuibia?
MSICHANA: Una maana gani?
MIMI: Hahahaha! Acha utani. Usitake nianze kutoa maana moja kwa moja hadi watu wa facebook washtukie.
MSICHANA: Kama yeye mwizi, sina budi nami kuwa mwizi.
MIMI: hauoni dhambi kuiba?
MSICHANA: Kwenye mapenzi sidhani kama kuna dhambi kuiba. Anayeua kwa upanga nae atauawa kwa upanga.
MIMI: Mmmhh! Sawa. Ila samahani kidogo. Kuna swali nataka kukuliza.
MSICHANA: Kuwa huru
MIMI: Unaonekana kuwa msichana wa tofauti sana. Yaani sio aina ya msichana ambaye amekulia hapa.
MSICHANA: Yeah! Nimeishi sana nchini Marekani ambako huko nilikaa kwa muda mrefu sana na ndipo nikalilia kuja Tanzania.
MIMI: Mmmh!
MSICHANA: Mbona unaguna tena?
MIMI: Hakuna bhana.
ENDELEA KUSOMA >>>>>>>>>>>>

Related

HADITHI 4505226079737818981

Post a Comment

ads by blogger

Follow Us

Hot in week

BLOG ZINGINE

BLOG OWNER

BLOG OWNER
MESHACK JACKSON

Side Ads

Instagram

JOIN US ON TWITTER

Text Widget

Millard Ayo – Official Website

item