MWANASHERIA MKUU AAHIDI KUANZA NA MIKATABA TATA

Dar es Salaam. Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), George Masaju amesema ataanza kuipitia mikataba yote inayodaiwa kuwa na utata ili aweze kutoa ufafanuzi wa kina lakini akawataka Watanzania wampe muda.
Hata hivyo, alisema hadhani kama watu wanaosema kuwa baadhi ya mikataba iliyoingiwa na Serikali ina utata wako sahihi na kuwataka Watanzania kuwa na imani na Serikali iliyopo madarakani.
“Watu wanasema hivyo ila kuna jambo moja ambalo wanatakiwa kujua kuwa kuna baadhi ya mikataba ambayo ni siri,” alisema.
Masaju aliteuliwa na Rais Jakaya Kikwete mwishoni mwa wiki kuchukua nafasi ya Jaji Frederick Werema ambaye alijiuzulu kutokana na sakata la Akaunti ya Tegeta Escrow.
Jaji Werema aliomba kujiuzulu kwa sababu ushauri wake kuhusu suala hilo haukueleweka na badala yake kuchafua hali ya hewa.
Kabla ya uteuzi huo, Masaju alikuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Kuhusu uteuzi wake, alisema; “Nina furaha kwa sababu ninalitumikia Taifa na kuteuliwa kwangu kunaonyesha kuwa Serikali ina imani na mimi.”
Licha ya kubanwa na wanahabari kuwa kwa nafasi aliyokuwa nayo awali anafahamu maeneo yenye matatizo, ikiwamo na mikataba yenye utata, alisisitiza kuwa apewe muda zaidi.
Katika mkutano wa 16 na 17 wa Bunge uliohitimishwa Novemba 28 mwaka jana, Bunge lilitoa maazimio manane, likiwamo la Jaji Werema kuwajibishwa kwa mujibu wa sheria kutokana na kuipotosha Serikali kuhusu mabilioni ya fedha kutoka akaunti ya Tegeta Escrow.
Maazimio mengine yalikuwa ni kuwajibisha baadhi ya mawaziri na bodi ya wakurugenzi wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco).
Kutokana na maazimio hayo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi amesimamishwa kazi, aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka amefukuzwa kazi na kuteuliwa kwa bodi mpya ya Tanesco.

Related

SIASA 6034579878497873607

Post a Comment

ads by blogger

Follow Us

Hot in week

BLOG ZINGINE

BLOG OWNER

BLOG OWNER
MESHACK JACKSON

Side Ads

Instagram

JOIN US ON TWITTER

Text Widget

Millard Ayo – Official Website

item